Kuhusu Sisi
Kuhusu Sisi

Fahamu Safari na
Malengo Yetu

Soma historia, dira, na dhamira yetu katika kuleta mabadiliko ya kifikra, kiuchumi na kijamii nchini Tanzania.

Mazingira yetu
Urithi na Mazingira

Kuhifadhi Mazingira
kwa Kizazi Kijacho

Tunasimamia miradi ya kupanda miti na kulinda vyanzo vya maji ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Safari Yetu

Historia ya Nyanyuka Afrika Foundation

Nyanyuka Afrika Foundation ni shirika lisilo la kiserikali lililosajiliwa rasmi tarehe 23/05/2025 (Na. 00NGO/R/8441), likiwa na makao makuu mkoani Dodoma, Tanzania.

Kuzaliwa kwa shirika hili ni matokeo ya vuguvugu la muda mrefu la harakati za kijamii za mwanzilishi Dotto Stephen Masulubu, kuanzia mwaka 2012 kupitia klabu za wanafunzi shuleni kama vile The Bright Family Club na The Orphan Students Association (OSA). Juhudi hizi zilichanua zaidi mwaka 2019 kupitia kampeni ya mtandaoni ya "Tukomeshe Mimba Shuleni" na kufikia kilele cha uzinduzi vya kampeni kubwa ya mazingira ya "Ziara Yangu, Mti Wangu" mnamo mwaka 2024 Ilizinduliwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini.

Lengo letu kuu ni kuendelea kutoa suluhisho endelevu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, changamoto za kiuchumi, na ukosefu wa ajira kwa vijana na wanawake kupitia misingi ya mageuzi ya kifikra (mindset change) na uwezeshaji wa vitendo.

Dira (Vision)

Kuwa taasisi ya kimotisha inayoongoza nchini Tanzania kwa kusaidia wananchi kuinuka kijamii, kiuchumi na kisiasa kupitia msaada wa kihali na mabadiliko ya fikra chanya.

Dhamira (Mission)

Kushughulikia changamoto za kijamii, kiuchumi na kisiasa kwa kutoa suluhisho kupitia ushirikiano na Serikali ya Tanzania, wananchi na wadau wa ndani na nje ya nchi.

Malengo Makuu (Objectives)

01

Kukuza maendeleo endelevu na uwezeshaji kupitia elimu, ujuzi wa kazi na ujasiriamali kwa vijana na wanawake.

02

Kuelimisha jamii kuhifadhi, kulinda na kusimamia rasilimali za asili na mazingira yanayotuzunguka ili kukabili mabadiliko ya tabianchi.

03

Kukuza utawala bora, haki za binadamu na utoaji wa elimu thabiti ya uraia kwa maendeleo ya taifa.

04

Kutoa msaada wa kisheria, ushauri, na elimu ya kisheria kwa makundi ya watu wasiojiweza na waliopo pembezoni mwa jamii.

Inua Jamii, Tunza Kesho

Mchango Wako Ndio Injini ya Mabadiliko

Kila shilingi unayochangia inakwenda moja kwa moja kununua miche ya miti, kutoa mafunzo kwa vijana, na kuimarisha mitandao ya kiuchumi ya kina mama na wafanyabiashara wadogo hapa Tanzania.

Wanaofanikisha Safari Hii

Washirika Wetu / Partners

TFS Tanzania TFS Tanzania
NEMC NEMC
Dodoma Jiji Dodoma Jiji
Dulaiki Group Dulaiki Group

Wasiliana Nasi

Je, una maswali, maoni au ungependa kushirikiana nasi? Timu yetu ipo tayari kusikia kutoka kwako wakati wowote.

nyanyukaafrikafoundation@gmail.com
+255 659 961 277 / +255 659 961 278
Cana Plaza, Dodoma | S.L.P 1249

Tuma Ujumbe wa Haraka