Matukio Yetu
Habari na Matukio

Ukurasa wa Mabadiliko

Fuatilia kwa karibu hatua, matukio, na taarifa zote za hivi punde kutoka kwenye miradi yetu ya kijamii na uhifadhi wa mazingira Tanzania.

Mazingira na Jamii
Taarifa za Uhakika

Ukweli na Ubunifu

Kila mradi tunaoutekeleza una lengo la kuleta ustawi wa kiuchumi na kijamii. Soma hapa kujionea nguvu ya ushirikiano.

Habari za Hivi Punde

News & Updates

Zote Zilizopita
Habari Matukio
10 July 2026

NYANYUKA AFRIKA FOUNDATION YATEULIWA KUSHIRIKI MRADI WA TACTIC WA UPANDAJI MITI MILIONI 2 JIJINI DODOMA

Dodoma, Tanzania — Nyanyuka Afrika Foundation imepata heshima ya kuteuliwa na kuwa miongoni mwa washiriki katika utekelezaji wa Mradi wa TACTIC, hususan katika programu ya upandaji miti na uhifadhi wa mazingira inayotarajiwa kutekelezwa katika Jiji la Dodoma. Programu hiyo inalenga kupanda miti milioni 2 ndani ya kipindi cha miaka miwili, ikiwa ni hatua muhimu katika kuongeza maeneo ya kijani, kuboresha mazingira ya Jiji la Dodoma na kuchangia juhudi za kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi. Katika maandalizi ya utekelezaji wa programu hiyo, Nyanyuka Afrika Foundation ilishiriki TACTIC Tree Planting Programme Workshop iliyofanyika Morogoro tarehe 9–10 Julai 2026. Taasisi hiyo iliwakilishwa na Dotto Stephen Masulubu, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mkuu wa Nyanyuka Afrika Foundation, aliyeshiriki pamoja na wadau mbalimbali katika kujadili maandalizi na utekelezaji wa mpango huo. Mradi wa TACTIC unatekelezwa kwa uratibu wa TARURA na kufadhiliwa na Benki ya Dunia (World Bank), huku ushiriki wa Nyanyuka Afrika Foundation ukiwa sehemu ya jitihada za kuunganisha nguvu za wadau katika kulinda na kuhifadhi mazingira. Nyanyuka Afrika Foundation imeeleza kuwa inathamini nafasi hiyo na iko tayari kushirikiana na TARURA, Serikali, Benki ya Dunia, wadau wengine pamoja na jamii ya Dodoma katika kuhakikisha lengo la upandaji miti linafikiwa. 🌱 Miti Milioni 2 kwa Dodoma Leo tunapanda miti, kesho tunajenga mazingira bora kwa kizazi kijacho. NYANYUKA AFRIKA FOUNDATION Mwanga wa Kila Kizazi 🌍

Habari Mazingira
June 2026

Kampeni ya "Ziara Yangu Mti Wangu" Yashika Kasi

Zoezi la ugawaji na upandaji miti limeendelea kwa mafanikio makubwa kwenye maeneo ya vyanzo vya maji.

Habari Urithi
May 2026

Mradi wa "Shitaka Urithi Mazingira"

Uhamasishaji wa jamii kuhusu utunzaji wa urithi wa asili na ulinzi wa wanyamapori dhidi ya uharibifu.

Kwenye Kalenda Yetu

Upcoming Events

HOT
15 Julai 2026
Dodoma Mjini

Kongamano la Kiuchumi la Vijana na Wanawake

Kukutana na kuwajengea uwezo wa kibiashara na fursa za mitandao kiuchumi wajasiriamali wadogo.

02:00 Asubuhi | Cana Plaza
Maelezo
08 Agosti 2026
Mazingira

Zoezi la Kitaifa la "Ziara Yangu, Mti Wangu"

Zoezi kubwa la kupandisha miti kwenye maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya kulinda vyanzo vya maji na kukabili ukame.

03:00 Asubuhi | Dodoma
Maelezo

Ofisi na Posta

Cana Plaza, Dodoma | S.L.P 1249 Dodoma

Simu

+255 659 961 277 / +255 659 961 278

Barua Pepe

nyanyukaafrikafoundation@gmail.com

Inua Jamii, Tunza Kesho

Mchango Wako Ndio Injini ya Mabadiliko

Kila shilingi unayochangia inakwenda moja kwa moja kununua miche ya miti, kutoa mafunzo kwa vijana, na kuimarisha mitandao ya kiuchumi ya kina mama na wafanyabiashara wadogo hapa Tanzania.